MONDULI MAASAI MARATHON YANOGA - JAMII BLOG

Jamii Yetu , Maisha Yetu

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday 1 July 2019

MONDULI MAASAI MARATHON YANOGA




 MWANARIADHA Magdalena Shauri akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon yaliyofanyika juzi wilayani hapo.(Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)
 MWANARIADHA  Marco Joseph akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon yaliyofanyika juzi wilayani hapo.


 MWANARIADHA  Asha Samwe akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon nafasi ya pili yaliyofanyika juzi wilayani hapo.
MWANARIADHA Josephat Joshua  akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon nafasi ya pili yaliyofanyika juzi wilayani hapo


MWANARIADHA  Mayselina  Mbua  akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon nafasi ya tatu yaliyofanyika juzi wilayani hapo

MWANARIADHA Fabiano Joseph  akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu mara baada ya kun'gara katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon nafasi ya tatu yaliyofanyika juzi wilayani hapo

Mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu akizungumza katika mashindano hayo mara baada ya kukabidhi zawadi washindi walioongoza katika mashindano ya riadha


Mmoja wa waandaaji wa Monduli Maasai Marathon  Meja Humphrey Nyuchi ambaye ni mkurugenzi mwenza alisema lengo hasa za mbio hizo kuimarisha michezo ,elimu na afya na mbio hizo zililenga katika kutangaza vivutio na fursa zilizopo Monduli.

Kikundi cha ngoma  kabila maarufu la kimaasai kikitoa  burudani katika mashindano hayo,

Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends Isabella Mwampamba akitoa zawadi shilingi elfu ishirini kwa mama aliyeshiriki mashindano hayo ya riadha huku akiwasii wanawake kujitokeza kwa wingi kushiriki michezo

Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends Isabella Mwampamba akiwa katika picha ya pamoja na watoto walioshiriki mashindano hayo,amabapo alidhamini Zawadi za watoto zenye thamani ya shilingi laki tatu

Kikundi cha Arusha runners wakishangilia zawadi ya mbuzi (2)walizokabidhiwa mara baada ya kutajwa kuwa wahamasishaji wa zuri wa shindano hilo


Na PamelaMollel,Monduli
Mashindano ya riadha maarufu kwa jina la Monduli Maasai Maradhon imekuwa kivutio kikubwa kwa wananachi waliojitokeza kuangalia shindano hilo lililowashirikisha wadau mbalimbali 
Mashindano hayo ya riadha yaliyofanyika juzi yanatajwa kuwa mashindano ya kwanza kufanyika Monduli na kufanya washiriki mbalimbali walioshinda kujinyakulia zawadi 
Wanariadha  Marco Joseph na Magdalena Shauri wamefanikiwa kushika nafasi ya kwanza  katika mashindano ya riadha ya Monduli Maasai Marathon
Kwa wanaume waliokimbia kilomita 21 Joseph Kutoka talenti alitumia Muda wa saa 1:19:27 akifuatiwa na Josephat Joshua Kutoka Polisi kwa muda wa 1:05:54  huku nafasi ya tatu akishilia Fabiano Joseph kutoka JWTZ kwa muda wa saa 1:06:13.
Kwa wanawake Magdalena Shauri aliongoza kwa muda wa saa 1:19:27 akifuatiwa na Asha Samwe kwa muda wa saa 1:20:16 huku nafasi ya tatu ikimwendea Mayselina  Mbua kwa muda wa 1:20:32.
Zaidi ya wanariadha 200 walishiriki mbio hizo za km 21,km 5 na km 2.5 ambazo ziliongozwa na mkuu wa wilaya Monduli Idd Kimanta ambapo washindi walikabidhiwa Zawadi za fedha na medali na tishirt.
Washindi kwa kilomita 21 kwa wanaume na wanawake ,Mshindi wa kwanza Alipata  shilingi laki 500,000 na ,mshindi wa pili 300,000 na   Mshindi  wa tatu 200,000, Mshindi  wa nne  150,000 na Mshindi  wa Tano 100,000 pamoja na katoni za vinywaji huku Zawadi za mbuzi mnyama zilitolewa kwa baadhi ya washindi wengine.
Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya  Monduli Meneja wa benki ya NMB Monduli  Rebecca Lobulu aliwapongeza waandaaji na washiriki,huku akisistiza kuwa michezo ni fursa ya ajira na pia inaimarisha mwili
Alitoa wito kwa wazazi kuwahimiza wototo michezo na badala yake waache kubeza watoto wanaofanya vizuri katika michezo
 Mmoja wa waandaaji wa Monduli Maasai Marathon  Meja Humphrey Nyuchi ambaye ni mkurugenzi mwenza alisema lengo la mashindano hayo kuibua fursa zilizopo katika eneo hilo pamoja na kuimarisha michezo
Alisema ni Mara ya Kwanza mbio hizo zinazinduliwa na matarajio mbio hizo zitakuwa endelevu kwa ila maana ya kuwa zitafanyika kila mwaka mwishoni mwa mwezi Juni .
Naye mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends Isabella Mwampamba ambaye walidhamini Zawadi za watoto zenye thamani ya shilingi laki tatu alisema kupitia michezo watotonwanaweza kufanya vizuri zaidi
Alisema serikali iweke mkazo zaidi kuwekeza katika michezo kuanzia ngazi za chini ili kuweza kuwa na vijana watakaofanya vizuri baadae na kuliwakilisha taifa vyema.
Mwisho

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here