Mteja kutoka Simanjiro alipata fursa ya kutembelea banda la ALAF katika maonyesho ya nane nane kanda ya kaskazini Arusha, akaeleza ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kampuni ya ALAF ambapo amewataka watanzania kupenda na kuthamini bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na kampuni hiyo kwa kuwa zinaubora wa hali ya juu(Habari picha na Pamela Mollel Arusha)
Afisa Masoko wa kampuni ya ALAF jijini Arusha Finias Wanguba akionyesha bati aina yaTekdek inayozalishwa na kampuni hiyo jijini Arusha,
Meneja mauzo kanda ya kaskazini Edward William akionyesha aina ya mabati yanayopatikana katika kampuni yao
Wateja wakiwa katika banda la kampuni ya ALAFwakipewa maelezo juu ya ubora wa bidhaa hiyo
Kampuni ya ALAF inayozalisha na kusambaza mabati ya aina mbalimbali
Na Pamela Mollel,Arusha
Kampuni ya
ALAF inayozalisha na kusambaza mabati ya aina mbalimbali ya rangi pamoja na bati maarufu simba dumu imekuwa
ikihudumia watanzania kwa zaidi ya miaka 50
Akizungumza
katika maonyesho ya nanenane kanda ya kaskazini Afisa Mauzo wa kamapuni ya ALAF
Finias Wanguba alisema kuwa mabati hayo
yana ubora wa hali ya juu na bei zake ni za kawaida tu hivyo mwananchi yeyote anaweza kumudu kununua
Pia katika
maonyesho hayo ya nanenane kamapuni hiyo imetoa punguzo la bei katika bidhaa
zake
Mabati haya
hupatikana kanda ya kaskazini Arusha,kanda ya kati Dodoma,kanda ya ziwa
Mwanza,Nyanda za juu kusini Mbeya,Dar esaalam
Hata hivyo
kiwanda cha ALAF ni kiwanda cha kwanza Tanzania kilicholeta teknologia ya bati
la msauzi ambapo huzalisha bati na chuma
Kwa upande
wake Mteja kutoka Simanjiro alipata fursa ya kutembelea banda la ALAF
katika maonyesho ya nane nane Mkoa Arusha, alieleza ubora wa bidhaa
zinazozalishwa na kampuni ya ALAF ambapo amewataka watanzania kupenda na
kuthamini bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na kampuni hiyo kwa kuwa zinaubora
wa hali ya juu
No comments:
Post a Comment