WATUHUMIWA WA UGAIDI BAADHI WAGOMA KUSHUKA KATIKA GARI LA MAGEREZA - JAMII BLOG

Jamii Yetu , Maisha Yetu

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday 25 April 2017

WATUHUMIWA WA UGAIDI BAADHI WAGOMA KUSHUKA KATIKA GARI LA MAGEREZA

Mahabusu wanaotuhumiwa na ugaidi jijini Arusha leo baadhi yao  wamegomea kushuka katika gari la magereza
kwa madai kuwa hawatendewi haki kwa kesi zao kutosikilizwa hali inayowalazimu kukaa mahabusu kwa muda mrefu bila kujua hatima yao

Watuhumiwa wa ugaidi baadhi yao wakiingia katika gari la magereza baada ya 32 kutii amri ya mahakama
Watuhumiwa wa ugaidi wakiwa katika viwanja vya mahakama leo jijini Arusha




Na Pamela Mollel,Arusha

Katika hali isiyokuwa ya kawaida  Mahabusu wanaotuhumiwa na ugaidi jijini Arusha baadhi yao leo wamegomea kushuka katika gari la magereza kwa madai kuwa hawatendewi haki kwa kesi zao kutosikilizwa hali inayowalazimu kukaa mahabusu kwa muda mrefu bila kujua hatima yao

Tukio hilo lilitokea  katika viwanja vya mahakama majira ya saa 9:27 asubuhi ambapo tukio hilo lilisimamisha shughuli za mahakama kwa muda wa zaidi ya masaa mawili huku baadhi ya watuhumiwa wengine wa ugaidi wakivua nguo zao kushinikiza kesi zao kusomwa

Mahabusu 32 tu ndio waliokubali kushuka katika gari hilo na kuingia mahakamani huku 29 wakigomea kushuka na kubakia ndani ya gari hali iliyozua taharuki kwa baadhi wa watu walikuja kufatilia kesi hiyo

Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Nestory Baro aliwataka watuhumiwa hao kuwa wavumilivu, kwa kuwa kesi yao ipo katika hatua za mwisho huku akiwasii kutogomea kuja mahakamini kwa kufanya hivyo wanajinyima haki yao ya kisheria

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mahakamani hapo watuhumiwa hao Shabani Idi na Yusuph Alli waliiomba mahakama kuharakisha kesi hiyo kwa kuwa familia zao zinaishi katika wakati mgumu 

“Mtoto wangu wa darasa la nne amekatisha masomo anaokota makopo kwaajili ya kuuza ili familia wapate chakula pamoja na wadogo zake kupata nauli ya shule”alisema Shabani 

Aidha waliongeza kuwa familia zao sasa zipo hatarini kuingia katika makundi mabaya ya tabia kutokana na wazazi wao kuwa mbali nao hivyo wao kuendelea kuwepo magerezani ni changamoto kubwa  sana kwa familia zao

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here