MKUU WA MKOA WA MWANZA AKUTANA NA WAGENI KUTOKA MAREKANI - JAMII BLOG

Jamii Yetu , Maisha Yetu

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday 3 October 2017

MKUU WA MKOA WA MWANZA AKUTANA NA WAGENI KUTOKA MAREKANI




Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella akizungumza na wageni/ watumishi wa Mungu kutoka taasisi ya More International Ministry ya Marekani ikiongozwa na Mwinjilisti Rojas Matias, walipomtembelea ofisini kwake jana.




Watumishi hao walikuwa na mkutano mkubwa wa injili tangu Septemba 27 hadi Oktoba Mosi, 2017 katika uwanja wa Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza ulioandaliwa na kanisa la EAGT Lumala Mpya chini ya Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola.




Mhe.Mongella aliwahakikishia ushirikiano mwema pindi watakapokuwa tayari kuwekeza katika shughuli mbalimbali ikiwemo za kielimu katika mkoa wa Mwanza.






Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella akizungumza na wageni/ watumishi wa Mungu kutoka taasisi ya More International Ministry ya Marekani



Wageni kutoka Marekani pamoja na mwenyeji wao Mchungaji Kulola, wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella.



Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (kulia) akizungumza na wageni/ watumishi wa Mungu kutoka taasisi ya More International Ministry ya Marekani. Katikati ni Mwinjilisti Rojas Matias kutoka Marekani na kushoto ni Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola kutoka kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza.



Baada ya mazungumzo, watumishi hao walifanya maombi kwa ajili ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza



Baada ya mazungumzo, watumishi hao walifanya maombi kwa ajili ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza



Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella (katikati), Mwinjilisti Rojas Matias kutoka Marekani (kushoto) pamoja na Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola kutoka kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza (kulia)



Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella (kushoto) akiwa pamoja na Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola kutoka kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza (kulia).



Katibu wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Levi Matia (kushoto), akiwakaribisha wageni kutoka Marekani walipotembelea ofisini hapo jana.



Timu ya More International Ministry kutoka Marekani ikiwa kwenye ofisi za mkuu wa mkoa wa Mwanza



Timu ya More International Ministry kutoka Marekani ikiondoka katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Mwanza na mwenyeji wao Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola (wa kwanza kushoto).



Salamu na wenyeji katika mitaa ya Jiji la Mwanza



Timu ya More International Ministry kutoka Marekani pamoja na wenyeji wao fukwe za Ziwa Victoria ili kujionea mawe ya "Bismarck Rock" katika eneo la Kamanga



Walifurahia uzuri wa eneo hili na hakika hii ni nenmbo ya Jiji la Mwanza



Walifurahia ukaaji wa mawe haya



Pia ilikuwa furaha kugusa maji ya Ziwa Victoria mubashara



Eneo hili lina mijusi wakubwa hivyo walifurahia kuitazama mubashara



Mwinjilisti Rojas Matias kutoka Marekani (kushoto) akiwa na mwenyeji wake Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola (kulia) kutoka kanisa la kimataifa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, katika fukwe za Kishimba Beach.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here